SHILOLE APANGA KUFANYA TIMBWILI 40 YA MTOTO WA NUH MZIWANDA



Shilole aka Shishi Trump ni mzungu. Amesema hana kinyongo na ex wake Nuh Mziwanda na ndio maana mwaliko wa 40 ya mtoto wa kike wa Nuh na mke wake Nawal ukihusika, ataenda kufanya makubwa.

“Mimi sinaga shobo ujue,” muimbaji huyo alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio hivi karibuni.

“Mimi naenda kwa moyo wangu kwamba ntaenda kama msanii mwenzangu kwamba hongera kwa kupata mtoto vizawadi hivi kama vibeseni, si unajua tena mama yake mkubwa wa zamani lazima naye.. sina tatizo,” aliongeza.

Alipoulizwa kwanini hakumpa mtoto Nuh kwenye uhusiano wao, staa huyo alijibu, ‘hatukujaaliwa tu.’ Shilole amesisitiza kuwa bado yupo single kwa sasa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MBINU 5 KALI ZA JINSI YA KUTONGOZA MSICHANA YOYOTE MREMBO NA AKUBALI

SPIKA NDUGAI AELEZEA MAANA YA NENO FALA

FAHAMU NJIA ZA KUSAIDIA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI