BUNGE;SPIKA NDUGAI ATOA YA MOYONI KUHUSU BAJETI YA SERIKALI MPYA



Spika wa Bunge, Job Ndugai ameionya Serikali juu ya ucheleweshaji wa uwasilishaji wa mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo waTaifa, kiwango na ukomo wa bajeti.

Akizungumza bungeni jana muda mfupi kabla ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango kuwasilisha mpango huo, Ndugai alisema kuwa kikanuni mpango huo unatakiwa kuwasilishwa Machi 11 ya kila mwaka.

“Kama ikiwa siku hiyo imeangukia siku isiyo ya kazi basi uwasilishaji huu hufanyika siku inayofuata. Mkija mwakani namna hii haitawezekana, hatutakuwa na mjadala,” alisema Ndugai.

Amewataka mawaziri, makatibu wakuu, maofisa wa Serikali na wabunge

kuhakikisha wanakuwapo mjini hapa kwa ajili ya kufanya uchambuzi wa mpango huo kisekta na kuhakikisha kuwa kazi hiyo inakamilika kabla ya kuanza kwa mkutano wa Bunge Aprili 4 mwaka huu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MBINU 5 KALI ZA JINSI YA KUTONGOZA MSICHANA YOYOTE MREMBO NA AKUBALI

SPIKA NDUGAI AELEZEA MAANA YA NENO FALA

FAHAMU NJIA ZA KUSAIDIA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI