LINAH ADAI WAZAZI WAKE WALIMKATAA MWANAUME ALIYEMPA UJAUZITO

Msanii wa muziki Linah Sanga ambaye kwa sasa ni mjamzito amefunguka kwa kudai kuwa wazazi wake walimkataa mpenzi wake wa sasa kwa kigezo cha dini.

Muimbaji huyo ambaye amelelewa katika misingi ya dini ya kikristo, amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds Fm kuwa haikuwa rahisi kwa wazazi wake kumkubali mwanaume huyo.

“Mwanzoni wazazi wangu walimkataa mpenzi wangu kisa ni dini tofauti na mimi, lakini sasa hawana pingamizi,” alisema Linah. “Tumeunganisha damu na kwenye mahusiano naamini upendo, nisingependa mtu anipangie, lakini jambo la wazazi kwa familia za kiafrika ni tofauti,”

Aliongeza, “Nimebeba ujauzito katika right time kwangu na mwenzangu yupo tayari. Mashabiki wategemee ndoa kabisa muda wowote.”

Muimbaji huyo kwa sasa anafanya vizuri na wimbo ‘Mfupi’ aliouachia hivi karibuni.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MBINU 5 KALI ZA JINSI YA KUTONGOZA MSICHANA YOYOTE MREMBO NA AKUBALI

SPIKA NDUGAI AELEZEA MAANA YA NENO FALA

FAHAMU NJIA ZA KUSAIDIA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI