CHINA NA KOREA KUSINI ZIMEIONYA PYONGYANG ENDAPO ZITALUSHA KOMBORA LOLOTE

Mataifa mawili ya bara Asia, yametoa onyo kali dhidi ya utawala wa Pyongyang, kwamba itaadhibiwa vikali, iwapo itadhubutu tena kufanyia majaribio zana zake za kinuklia.

Mataifa hayo, Korea Kusini na China, yamekiri kuchukua hatua kali dhidi ya Korea Kaskazini, ikiwa tena itafanyia majaribio zana zake za kitonoradi zinazovuka mipaka ya kimataifa.

Tangazo hilo linatukia baada ya mkutano uliofanyika Seoul, kati ya wajumbe wa China na Korea Kusini, na hatua ya Marekani ya kutumameli za kivita hadi katika maeneo ya maji kwenye rasi ya Korea.


Taifa la Korea Kaskazini mara kwa mara limekuwa likiimarisha uwezo wake wa kivita, licha ya kuwekewa vikwazo na Umoja wa mataifa.

Kwa kweli, majaribio hayo ya mara kwa mara, yameongezeka sana chini ya utawala wa Rais Kim Jong-un.

Rais Trump wa Marekani, ameahidi "kutanzua" Korea Kaskazini bila ya kusaidiwa na China, mshirika wa pekee wa Pyongyang.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MBINU 5 KALI ZA JINSI YA KUTONGOZA MSICHANA YOYOTE MREMBO NA AKUBALI

SPIKA NDUGAI AELEZEA MAANA YA NENO FALA

FAHAMU NJIA ZA KUSAIDIA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI