Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2017

TUNDU LISSU AKOMALIA VYETI FAKE VYA BASHITE

Picha
Wakili Tundu Lissu na wenzake wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS) wamelikomalia vilivyo sakata maarufu la Bashite linalohusiana na tuhuma za kughushi vyeti vya kielimu linalomkabili mmoja wa wakuu wa mikoa kwa kulifikisha kortini ili lipatiwe ufumbuzi. Aidha, Lissu na wenzake hao wamedhamiria kuona kuwa kigogo huyo anayetuhumiwa kuliacha jina lake halisi la Daudi Albert Bashite kutokana na matokeo mabovu ya sekondari na kutumia jina la mtu mwingine, achukuliwe hatua za kisheria ikiwamo kufungwa jela kwa kosa la kughushi ikiwa itathibitika kuwa ana hatia. Akizungumza jana na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, Lissu ambaye ni Rais wa TLS, alisema uamuzi huo wa kulifikisha mahakamani suala la Bashite umetokana na maazimio ya baraza la uongozi la chama hicho, lengo likiwa ni kulinda utawala wa sheria na uwajibikaji nchini. Tofauti na matarajio ya baadhi ya watu, sakata hilo la Bashite halikupatiwa jibu kutokana na ripoti ya uhakiki wa vyeti vya watumishi wote wa umma iliyokabi...

RAYVANNY AZITAJA COLLABO ZAKE ZA NJE

Picha
Msanii Rayvanny ametaja kolabo zake na wasanii wa nje ambazo zipo tayari. Muimbaji huyo, ambaye yupo nchini Sweden kwa ziara yake ya muziki, amemuambia mmoja wa watangazaji wa nchi hiyo kua, tayari ameshafanya kolabo na msanii mkubwa kutoka Nigeria, Afrika Kusini na Kenya. “Nina kolabo na msanii mkubwa kutoka Nigeria, ingawa kwa sasa siwezi kutaja jina lake. Lakini pia kuna kolabo Afrika Kusini, na Kenya ukiacha Bahati, kuna mwingine Khaligraph Jones kutoka Nairobi,” amesema Ray. Kwa msanii wa Afrika Kusini tayari muimbaji huyo kutoka WCB ameshafanya kolabo na Dj Maphorisa tangu mwezi Disemba mwaka jana.

NAPE ATOA USHAURI KWA WANANCHI

Picha
Mbunge wa jimbo la Mtama, Mh Nape Nnauye amemkumbuka marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuamua kutumia maneno yake katika kufikisha ujumbe wake kwa wananchi kupitia ukurasa wake wa twitter  Mhe Nape Nnauye alikuwa akitoa ujumbe kuwa maana ya ubinadamu na heshima ya binadamu ni kutokaa kimya pale jambo la uovu linapokuwa likitokea, akiwataka wananchi kutokaa kimya wanapoona kuna jambo la uovu linatendeka. Ili kufikisha ujumbe huo vizuri Mhe. Nape Nnauye ilibidi atumie clip ya video ya marehemu baba wa taifa, Julius Kambarage Nyerere wakati akihotubia kwa mara ya mwisho katika Mkutano Mkuu. Ambapo mwalimu alisema maneno haya kwa lugha ya kiingerza   "Hotuba yangu ya mwisho kwenye huu mkutano mkuu, nimeelezea matukio na mienendo na mahitaji kwa namna ambavyo sisi Watanzania tuonavyo, kukaa kimya pale tuonapo hatari, kutulia tu pale tuonapo sera hatari ambazo ziko kinyume na kulinda amani na haki, kufanya hivyo itakuwa tunaachia uhuru wetu na utu wetu ...

MAGAZETI YA LEO 1/5/2017

Picha

NIKKI WA PILI AMCHANA RAY

Picha
Msanii wa hip hop nchini Tanzania Nikk Wa Pili amesema kuwa mastaa wengi wa Bongo Movie tunawafahamu sana kuliko kazi zao tofauti ilivyo kwa wasanii wa filamu za nje. Nikk Wa pili alizungumza hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Friday Night Live (FNL)  nakusisitiza kuwa mastaa wengi wa bongo wanatrendi kwa muda mrefu hata zaidi ya miaka mitatu (3) kwa mambo mengine lakini movie zao hazijulikanii kabisa.  "Ni kweli mastaa wengi wa movie Tanzania tunawafahamu sana wao kuliko kazi zao, kuna mtu unamsikia na unamuona anatrendi kwa miaka mitatu lakini hauijui movie yake hata moja" alisema Nikk Wa Pili. Nikk ametoa mfano wa kupitia msanii maarufu wa Bongo Movie nchini  Ray Kigosi na kusema hafahamu movie yake hata moja lakini ishu yake kama ile ya kuywa maji sana aliisikia na ilitrendi kweli kweli. "Sizifahamu movie za Ray Kigosi lakini ishu yake ya maji naijua, ile ishu kwamba anakunywa sana maji niliisikia sana lakini movie zake sizijui" - alisisitiza Nikk Wa Pili. ...

NIVA AMFUNGUKIA NEY WA MITEGO ASEMA ANATUMIA MADAWA

Picha
Msanii wa muziki wa bongo fleva Shiloe alimaarufu kama Shishi Baby amefunguka na kuwataka wanaume ambao wanategemea wanawake kuvalishwa, kulishwa wabadilike na kuanza kufanya kazi ili wasitegemee tena wanawake kuendesha maisha yao. Niva alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Friday Night Live (FNL) na kusema hiyo ndiyo sababu kubwa msanii huyo amekuwa anakimbia mapambano kila anapoombwa wazipange , lakini pia Niva anasema Nay wa Mitego anatafuta kiki kupitia bongo movie. "Nay anapokuwa anaingia studio au kutoa wimbo mpya ndiyo amekuwa akiichokoza bongo movie ili apate kiki, Nay ni mtu ambaye hana heshima halafu kwa wachache wanaomuogopa ndiyo wanatia kiburi labda vile vijitu vyake anavyovimiliki sijui producer, meneja ndiyo wanamtia kiburi. Sisi huku bongo movie tunafanya kazi kubwa zaidi yake yeye. Mimi Nay wa Mitego namjua nguvu yule hana,  Nay hana mazoezi ule mwili anakula madude  (madawa) yao ya kukuza mwili, Nay hana mazoezi mimi ndiyo namjua Emma Chogo"  Ali...

ZITO KABWE AFUNGUKA MAZITO JUU YA NDEGE MPYA ZA BOEING

Picha
Sakala la Serikali kusemekana imenunua ndege ya Boeing ambayo ina walakini imechukua sura mpya baada ya Mbunge Zitto Kufunguka Haya Hapa chini kupitia page yake ya Facebook: "Hizi Ndio Habari za kina kuhusu ndege ya Boeing 787 Dreamliner tuliyokwishalipia. Ni sehemu ya ndege zilizokuwa chini ya kiwango zikiitwa Terrible Teens. Iliundwa mwaka 2009 na kununuliwa na ReandAir Tarehe 21/11/2013. Baada ya Mwaka, tarehe 3/12/2014, Rwanda wakaikataa na kuirudisha. Tanzania imeinunua tarehe 14/12/2016 Kwa dola za kimarekani 224 milioni.  Sasa, mwanzo nilitaka maelezo ya Serikali, wasemaji wa Serikali wakawa wengi Sana kuwa tuliyonunua sisi sio terrible tween. Nimefanya utafiti kidogo na NIMETHIBITISHA kuwa tumenunua ndege zilizokatawaliwa hata na Rwanda rafiki zetu. Kinachofuata ni kikubwa zaidi. Watetezi wa Serikali muwe tayari kuja kutetea pia maana labda mna mgawo. Kifuatacho NCHI ITATIKISIKA"  Zitto Kabwe

FROLA MBASHA HAPENDI MAISHA YA USTAA

Picha
Madam Flora (zamani Flora Mbasha) amesema hayo hivi karibuni ikiwa ni siku chache kuelekea ndoa yake ambapo amefunguka na kudai kuwa baada ya kumpata mwanaume ambaye siyo maarufu anafurahi kwani hata mfumo wa maisha yake utaenda kubadilika na kuishi kama watu wengine ambao siyo maarufu. "Mume wangu mtarajiwa siyo mtu anayejulikana  bali naamini kwenye ulimwengu wa kiroho anajulikana. Namshukuru Mungu maisha mapya ambayo naenda kuyaishi siyo ya umaarufu. Mimi nimemwambia pamoja na ustaa nilionao napenda tuishi maisha ya kawaida ambayo hayahusiani na umaarufu wangu. Unajua kuna wakati natamani kushuka kwenda kula chakula kwa mama n'tilie lakini watu watashangaa hata wewe? sasa najiuliza who is Flora?  kumbe mimi pia ni mtu wa kawaida kabisa. Sitamani maisha ya Ustaa yananinyima uhuru"- Madam Flora. Aidha Flora amefunguka kuhusu mahusiano yake na kwamba kabla ya kukubali kuolewa kwa mara ya pili ilimchukua zaidi ya mwaka mmoja kutafakari ikiwa ni pamoja na kushirikisha fa...

CHID BENZ AREJEA URAIANI

Picha
Msanii wa muziki wa hip hop, Chidi Benz amedai amejifunza vitu vingi kwa kipindi cha miezi mitatu alichokaa rehab mkoani Tanga na Iringa kwa ajili ya kusaidiwa kuacha matumizi ya dawa za kulevya.  Akiongea katika kipindi cha Clouds E cha Clouds TV, Chid Benz amedai kukaa rehab kwa miezi mitatu bila tatizo ni mafanikio mapya katika maisha yake.  “Nimejifunza vitu na ninaendelea kujifunza vitu,” alisema Chidi. “Nimekaa muda mrefu zaidi maana sijawahi kukaa rehab miezi mitatu na ndio maana unaona nimetulia mpaka sasa hivi. Nina miezi miwili toka nimetoka niko poa niko freshi,”  Katika hatua nyingine rapa huyo amemtaka mwanaharakati wa kupambana na dawa za kulevya, Kalapina, kujifunza mbinu mpya ili aweze kuwasaidia vijana wa aina mbalimbali ambao wanakumbwa na tatizo hilo.

NEY WA MITEGO SIFUNDISHWI WALA SIPANGIWI CHA KUONGEA

Picha
Msanii wa Bongo fleva Nay wa Mitego amefunguka mapya na kusema yeye hana muda wa kupoteza wa kupigana na msanii wa bongo 'movie' Yusuph Mlela huku akijitapa kuwa hapangiwi wala hafundishwi jambo analotaka kuongea. Nay ameeleza hayo baada ya kuambiwa na Mlela ajiheshimu na asiingilie kazi za watu ambazo hazimuhusu huku akisisitiza kwamba kama angekuwa anaimba basi angeingia studio ili atangeneze wimbo wa kumchana lakini kwa vile kazi zao haziingiliani alimtaka wapande ulingoni wazichape waweze kutengenezeana  heshima kati yao na siyo kupiga maneno tu. "Mimi ni Baba mwenye watoto, mimi ni mtu  mwenye familia 'so' ukiwa unataka kuniuliza kitu angalia watu wa kuniweka nao ....Usiniweka na watu ambao unaona kabisa hiki siyo sawa. Mimi naongea na bongo 'movie' wote...Mimi nipo 'free' sana nipo huru kuongea jambo lolote...Mimi napenda kuongea ukweli, wewe unaweza kukataa nilichokiongea lakini asilimia kubwa wanaelewa ninachoongea 'thats why' nik...

MAGAZETI YA LEO APRIL 30/2017

Picha