Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2017

MAGAZETI YA LEO JUNI 1/2017

Picha

YERICKO NYERERE AKAMATWA NYUMBANI KWAKE WACHUKUA SIMU NA LAPTOP

Picha
Watu waliojitambulisha kuwa ni Polisi kitengo cha cyber crime! Wamefika mda huu majira ya saa 7:04 usiku, Kwa Yericko Nyerere wakiambatana na mwenyekiti Wa mtaa (Mbutu), walipofika wamemchukua yeye pamoja na vifaa vyake ikiwemo simu na laptop yake na kuondoka naye kuelekea kituo cha police kigamboni wakimtuhumu kuhusika na kosa la kimtandao.(ingawa hawakueleza kosa halisi kafanya lini na wapi). Taarifa zaidi mtaendelea kuzipata baadae. Ikumbukwe hii ni Mara ya pili kukamatwa kwake, baada ya kesi yake iliyodumu Kwa miaka miwili tangu kipindi cha uchaguzi ambapo alishinda na kuachiwa huru mapema April 2017. UPDATES: Taarifa zilizonifikia hivi punde nikwamba; kituo cha kigamboni hakija mshikilia Yericko, na wala hawajui alikamatwa Kwa kosa gani; kutokana na taratibu za kazi wao kama polisi. Wenyeji walitoa ushirikiano kutokana na jiografia ya eneo analoishi Yericko kuwa ni porini pembezoni mwa mji, kiasi kwamba Kwa gari yao (oppa) waliokuja nayo, isingekuwa rahisi kufika, Kigamboni...

LEMA ATAKA KAMBI YA UPINZANI IVUNJWE

Picha
MBUNGE wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbles Lema (Chadema), amelitaka Bunge kuvunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kutokana na maoni ya kambi hiyo kutosikilizwa. Aidha, Lema amedai kuna kuchujwa kwa maneno yanayochangiwa na wabunge wa kambi hiyo katika mijadala katika taarifa za kumbukumbu za Bunge(hansard), alikodai kunafanywa na wafanyakazi wa Studio ya Bunge. Aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana asubuhi aliposimama na kuomba mwongozo wa Kiti cha Spika akidai kuwa michango ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikihaririwa na baadhi ya maneno yamekuwa yakiondolewa na hivyo kutorushwa kwenye studio hiyo na hata kwenye taarifa wanazopewa waandishi wa habari wa redio na televisheni. Hata hivyo, katika mwongozo wake kuhusu suala hilo muda mfupi kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge jana mchana, Mwenyekiti wa Bunge, Najma Murtaza Giga, aliyekuwa akiongoza kikao cha jana, alisema Studio ya Bunge haina utaratibu wa kuchuja michango ya wapinzani isipokuwa kwa maelekezo ya Kiti cha Sp...

PROF;MUHONGO AWATOA HOFU WAPIGA KURA WAKE BAADA YA KUFUTWA KAZI

Picha
MARA: Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini na Mbunge wa Musoma Vijiji Prof. Sospeter Muhongo amewasihi wakazi wa jimbo hilo kutokuingiwa na hofu kufuatia uamuzi wa Rais Dkt Magufuli kumfuta kazi. Prof. Muhongo amewataka wapigakura wake na rafiki zake kutokuwa na hofu kwani kwa pamoja watafanikiwa. Kwa mujibu wa taarifa za ofisi yake, amewaahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha kuwa wanafikia malengo yao ya kimaendeleo kwa kutimiza ahadi zake. Taarifa hiyo ilitolewa na Katibu wa Mbunge huyo, Juma Ramadhan ambaye alisema kuwa kilichotokea ni cha kawaida kwenye siasa na inawapasa kusahau hayo ili waweze kusonga mbele katika kutekeleza miradi ya maendeleo. Kwa sasa tunajielekeza kujenga vyumba vya madarasa na miradi mingine ya maendeleo, hivyo ni vyema tukaungana pamoja ili kuweza kutekeleza majukumu haya, alisema msaidizi huo. Wakazi wa jimbo hilo waliahidi kutoa ushirikiano kwa mbunge wao katika kutekeleza miradi hiyo kwani yeye si kiongozi wa kwanza kuondolewa kwenye wadh...

KAIRUKI ASEMA SERIKALI HAITA AJIRI WALIMU WA MASOMO YA SANAA

Picha
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki amefunguka na kusema serikali kwa sasa haitaweza kuajiri walimu wapya wa sanaa bali itawatumia walimu wa sanaa wa ziada waliopo katika shule za sekondari. Angela Kairuki amesema hayo leo bungeni na kudai kila shule itaweza kupata walimu wa sanaa kulingana na mahitaji yao "Utafiti uliofanywa na Ofisi ya Rais Tamisemi mwaka 2015/2016 umebaini kuwepo kwa ziada ya walimu wa masomo ya sanaa wapatao 7463 katika shule za sekondari, kutokana na hali hii serikali inaendelea na zoezi la kuwagawanya walimu hao au kuwa 'redeploy' kwa kuzingatia uwiano na mahitaji halisi ya walimu wa sanaa kwa kila mamlaka za serikali za mitaa ili kila shule iweze kupata walimu wa masomo ya sanaa badala ya kuajiri walimu wapya" -alisema Angela Kairuki Mbali na hilo Waziri Kairuki amesema serikali inaendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali ambapo katika mwaka wa fedha 2016/2017 watumishi zaidi ya elfu tisa wameajiriwa ...

PICHA ZA BEN PAUL ZAMPA DILI

Picha
Msanii wa Bongo Fleva, Ben Pol amefunguka kwa kusema kuwa baada ya kusambaza mtandaoni picha zinazomuonyesha akiwa nusu mtupu na mng’ao wa mafuta, sasa amepata dili ya kuwa balozi wa mafuta ya kujipaka na kwa sasa wapo kwenye hatua za mwisho za mazungumzo. Ben Pol amekimbia kipindi cha Kwetu Flavor ya Magic Fm kuwa baada ya picha kusambaa, kuna makampuni yamemfuata  na kutaka kufanya naye biashara ya matangazo. “Hapa sasa hivi tunaongea kuhusu majukumu yangu kama balozi, nione nina show ngapi katika hiyo event na mambo ya maslai inakuaje, nione matangazo ya runinga na mabango na nijue amount ya kazi yote ilivyo ni kiasi gani ninaweza kunufaika.Tukifikia muhafaka watu wataniona kwenye mabango, nimekoleza mafuta nimeweka na logo za hiyo kampuni,” amesema Ben Pol.

MAGAZETI YA LEO MEI 31/2017

Picha