RAIS KENYATA AWAOMBEA WANAFUNZI 33 WALIOPATA AJARI TANZANIA

Rais wa Jamhuri ya Kenya, Uhuru Kenya amewaongoza raia wa nchi hiyo jana katika kuomboleza vifo vya wanafunzi 33 vilivyotokea Wilayani Karatu, Mkoa wa Arusha nchini Tanzania.

Kenyatta ambaye ni mgombea wa kiti cha urais kwa tiketi ya muungano wa Jubilee, aliwaomba raia wa Kenya kusimama kwa dakika moja kuomboleza na kuwaombea wanafunzi 33, walimu 2 na dereva waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea jana saa tatu asubuhi.

Rais Uhuru alitoa heshima hiyo alipokuwa katika moja ya mikutano yake ya hadhara nchini humo ambapo anatetea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti mwaka huu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MBINU 5 KALI ZA JINSI YA KUTONGOZA MSICHANA YOYOTE MREMBO NA AKUBALI

SPIKA NDUGAI AELEZEA MAANA YA NENO FALA

FAHAMU NJIA ZA KUSAIDIA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI