GODZILLA KAWACHANA NIKKI MBISHI NA WAKAZI

Msanii wa muziki wa hip hop nchini, Godzilla amefunguka kwa kuwachana wasanii wenzake wanaoishi Ukonga Jijini Dar es Salaam kwa kuwaambia ni miyeyusho japokuwa ni ndugu zake wa kipindi kirefu na bado anawalea.

Zilla amesema hayo baada ya kuulizwa chanzo cha ugomvi wake na msanii Nikki Mbishi pamoja na Wakazi.

“Nikki ‘is my friend’ tumefanya kazi kwenye nyimbo yake, ‘I don’t know’ sijui kitu gani kimetokea lakini ‘we still friend. Mimi sina tatizo kwa sababu kama ingekuwa chochote kimetokea watu tusingefanya kazi pamoja, lakini imekuwa ‘too much’,” Zilla alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV.

“Unajua watoto wa Ukonga wengi wanakuwa miyeyusho miyeyusho lakini ni ndugu zangu wakina Wakazi, Nikki tunawalea tutafanyaje wanetu hao” aliongeza.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MBINU 5 KALI ZA JINSI YA KUTONGOZA MSICHANA YOYOTE MREMBO NA AKUBALI

SPIKA NDUGAI AELEZEA MAANA YA NENO FALA

FAHAMU NJIA ZA KUSAIDIA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI